KOZI FUPI YA UENDESHAJI MITAMBO  ITAKAVYOWAOKOA WAHITIMU VETA

Na Aziza Masoud,Dar es Salaam

MAMLAKA ya  Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imewataka wahitimu wa shule za sekondari pamoja na wafanyakazi waliopo viwandani kujiunga na chuo hicho kusomea  kozi zakuendesha mitambo na machine za viwandani.

Akizungumza leo Julai 4, ,2025atika Maonesho ya Biashara ya 49 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DTIF) maarufu kama Saba Saba Mkufunzi Kutoka Veta tawi la  Kipawa Joshua Mwankusye alisema  mamlaka inatoa mafunzo ya mifumo yakuendesha mashine ziweze kufanya kazi wenyewe.

“Kuna kozi fupi kuna system ya mifumo  yakuendesha mashine zifanye kazi zenyewe kwa msaada kidogo,ni  kozi ya muda mfupi wa miezi miwili anakuwa qualified  baada ya hapo ataenda field viwandani kwa ajili yakuboresha alichojifunza,”alisema Mwankusye.

Alisema kozi hiyi kwa VETAni muhimu kwakuwawat7 wengi huwa wanaenda kuisoma nje ya nchi tena kwa gharama kubwa  tofauti na VETA ambapo inapatikana kwa gharama nafuu.

“Wengi waliokuja ni tayari wameshapata kazi,muitikio wa wanafunzi bado mdogo kwakuwa wazazi kwakuwa bado hawajaelewa vizuri tunapowaambia kozi itawasaidia kupata ajira na kujiajiri,*alisema.

Alisema mpaka sasa jumla ya wanafunzi  35 wameshahitimu kozi hii tangu ilipoanzishwa mwaka juzi .