MAENEO YALIOATHIRIWA NA MVUA BARABARA YA DAR-LINDI-MTWARA YOTE NI SHWARI
Barabara ya Dar es salam-Lindi-Mtwara sasa imerejea katika hali ya kupitika baada ya kukamilika urejeshaji…
Na Mwamdishi Wetu,Dodoma MKURUGENZI wa Huduma za Udhibiti wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) , Daniel Ndiyo amewataka wananchi kuzitumia maabara za Mamlaka kuchunguza mazao ya kilimo ili kutambua usalama wake kabla ya matumizi. Mkurugenzi Ndiyo amesema hayo Agosti 7, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa Habari waliotembelea Banda la Mamlaka…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma MWENYEKITI wa Bodi ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Bi. Yokbeth Festo Myumbilwa, amesema tafiti za jiosayansi zinazofanywa na taasisi hiyo zina mchango mkubwa katika kuibua maeneo yenye rasilimali za madini, kuvutia uwekezaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa unaolengwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050….
Na Mwandishi Wetu,Dodoma WAKALA wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umesema umejizatiti kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na upatikanaji wa uhakika wa mafuta wakati wote kupitia mfumo wa uagizaji wa pamoja, hatua inayochangia ukuaji wa uchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Akizungumza leo Agosti 7, 2026 katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma SERIKALI kupitia Tume ya Madini imefungua fursa za biashara zenye thamani ya mabilioni ya fedha katika migodi kwa Watanzania, huku vijana na wanawake wakipewa kipaumbele ili kuongeza ushiriki wao katika Sekta ya Madini na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Hatua hiyo inalenga kujenga uchumi shindani na jumuishi unaowezesha…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma Mfumo wa kuagiza mafuta kwa ajili ya matumizi ya miezi miwili inayofuata umeiwezesha Tanzania kuendelea kuwa na bidhaa za mafuta za kutosha, licha ya vita na changamoto nyingine zinazoathiri soko la dunia. Hayo yameelezwa na Mhandisi Rehema Mahundi katika siku ya sita ya Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, wakati akitoa elimu…
Na Mwandishi Wetu, Dodoma BODI ya Bima ya Amana (DIB) imesema imeanza kutekeleza jukumu jipya la kusaidia benki na taasisi za fedha zinazokabiliwa na changamoto za kifedha ili zisifilisike, hatua inayolenga kulinda fedha za wateja na kudumisha utulivu wa sekta ya fedha nchini. Akizungumza katika Maonesho ya Wakulima ya Kimataifa Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya…
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Serikali imeongeza kasi ya utafiti wa madini nchini katika hatua inayolenga kufungua maeneo mapya ya uwekezaji, kuongeza ajira na mapato ya Serikali, huku wachimbaji wadogo wakitarajiwa kunufaika kwa kupata taarifa sahihi zitakazowasaidia kufanya uchimbaji wenye tija. Akizungumza katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa…
Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Wilaya ya Ubungo imeanza utekelezaji wa mpango wa kuboresha huduma ya maji katika Mtaa wa Kimara B kwa kulaza bomba lenye uwezo mkubwa zaidi, hatua inayolenga kukidhi mahitaji ya sasa ya wakazi na kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji…
Tume ya Madini yasisitiza uchimbaji unaozingatia sheria, afya na maendeleo endelevu Na Mwandishi Wetu,Dodoma TUME ya Madini imeendelea kuimarisha ukaguzi wa migodi nchini ili kuhakikisha shughuli zote za uchimbaji zinafanyika kwa kuzingatia sheria, usalama wa wafanyakazi, afya kazini na utunzaji wa mazingira, hatua inayolenga kujenga sekta ya madini yenye tija na endelevu. Akizungumza katika Maonesho…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma MKURUGENZI wa Nishati Jadidifu na Teknolojia Mbadala wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Advera Mwijage, amesema REA imeanza utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini ili kuboresha upatikanaji wa huduma za mafuta na kuchochea maendeleo ya shughuli za kiuchumi katika maeneo ya vijijini. Akizungumza na wadau waliotembelea…