MAENEO YALIOATHIRIWA NA MVUA BARABARA YA DAR-LINDI-MTWARA YOTE NI SHWARI
Barabara ya Dar es salam-Lindi-Mtwara sasa imerejea katika hali ya kupitika baada ya kukamilika urejeshaji…
Na Mwandishi Wetu, Dodoma CHUO cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kimesema kuwa Tanzania inahitaji kuongeza idadi ya wataalamu wa usafirishaji na usimamizi wa mnyororo wa bidhaa ili kuongeza tija, ushindani wa bidhaa za ndani na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Akizungumza wakati wa alipotembelea Maonesho ya Wakulima Nanenane ,Mkuu wa…
Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeweka mkakati wa kuchochea shughuli za kiuchumi nchini kwa kuwashirikisha wawekezaji katika ujenzi wa nyumba, majengo ya biashara, viwanda na miundombinu ya kuhifadhi na kuchakata mazao. Hatua hiyo inatajwa kuwa na uwezo wa kuongeza thamani ya mazao, kufungua masoko mapya kwa wakulima na wafugaji pamoja na…
Na Aziza Masoud, Dodoma CHUO Kikuu Cha Dodoma (UDOM) kimetengeneza mfumo wa kidijitali wa Ghala Project unaolenga kuongeza uwazi katika matumizi ya mfumo wa stakabadhi ghalani na kuwawezesha wakulima kupata taarifa za mazao yao kwa wakati. Mfumo huo unaotekelezwa kupitia Ghala Project, unalenga kutatua changamoto zinazowakabili wakulima katika kupata taarifa baada ya kuwasilisha mazao yao maghalani,…
Na Aziza Masoud, Dodoma WAKATI asali ikiendelea kuwa zao la nyuki linalofahamika na kutumiwa na Watanzania wengi, wazalishaji wa mazao ya nyuki wameanza kuhamasisha matumizi ya chavua ya nyuki (bee pollen), wakisema bado haijapata soko kubwa licha ya kuwa na virutubisho vinavyoweza kusaidia afya. Akizungumza katika banda la Benki ya Kilimo Tanzania (TADB) katika Maonesho…
Na Mwamdishi Wetu,Dodoma MKURUGENZI wa Huduma za Udhibiti wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) , Daniel Ndiyo amewataka wananchi kuzitumia maabara za Mamlaka kuchunguza mazao ya kilimo ili kutambua usalama wake kabla ya matumizi. Mkurugenzi Ndiyo amesema hayo Agosti 7, 2026 wakati akizungumza na waandishi wa Habari waliotembelea Banda la Mamlaka…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma MWENYEKITI wa Bodi ya Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Bi. Yokbeth Festo Myumbilwa, amesema tafiti za jiosayansi zinazofanywa na taasisi hiyo zina mchango mkubwa katika kuibua maeneo yenye rasilimali za madini, kuvutia uwekezaji na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa unaolengwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050….
Na Mwandishi Wetu,Dodoma WAKALA wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) umesema umejizatiti kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa na upatikanaji wa uhakika wa mafuta wakati wote kupitia mfumo wa uagizaji wa pamoja, hatua inayochangia ukuaji wa uchumi na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Akizungumza leo Agosti 7, 2026 katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma SERIKALI kupitia Tume ya Madini imefungua fursa za biashara zenye thamani ya mabilioni ya fedha katika migodi kwa Watanzania, huku vijana na wanawake wakipewa kipaumbele ili kuongeza ushiriki wao katika Sekta ya Madini na kuchochea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Hatua hiyo inalenga kujenga uchumi shindani na jumuishi unaowezesha…
Na Mwandishi Wetu,Dodoma Mfumo wa kuagiza mafuta kwa ajili ya matumizi ya miezi miwili inayofuata umeiwezesha Tanzania kuendelea kuwa na bidhaa za mafuta za kutosha, licha ya vita na changamoto nyingine zinazoathiri soko la dunia. Hayo yameelezwa na Mhandisi Rehema Mahundi katika siku ya sita ya Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Dodoma, wakati akitoa elimu…
Na Mwandishi Wetu, Dodoma BODI ya Bima ya Amana (DIB) imesema imeanza kutekeleza jukumu jipya la kusaidia benki na taasisi za fedha zinazokabiliwa na changamoto za kifedha ili zisifilisike, hatua inayolenga kulinda fedha za wateja na kudumisha utulivu wa sekta ya fedha nchini. Akizungumza katika Maonesho ya Wakulima ya Kimataifa Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya…