CPA KASOLE:KAMPUNI TANZU ITASAIDIA KUKUZA BUNIFU ZETU

Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo Stadi (VETA) imeanzisha kampuni tanzu ambayo inahusika na kukuza bidhaa  bunifu  zinazotengenezwa kupitia vyuo vyake mbalimbali.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurungezi Mkuu wa VETA, Anthony Kasole wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonesho ya 49 ya Kimataifa ya kibiashara Sabasaba yanayoendelea.

 CPA Kasole alisema VETA  imeanzisha   kampuni hiyo ambayo inahusuka na  kukuza bidhaa bunifu zinazotegenezwa kupitia vyuo vyake mbalimbali .

“Bidhaa zote ambazo zitakuwa zikitegenezwa na wanafunzi  kutoka katika vyuo hivyo zitakuwa zikiuzwa katika Kampuni hiyo tanzu,”

Alisema kampuni hiyo tanzu itakuwa ikihususika na bidhaa zote tunazozitegeneza pamoja na kutoa huduma mbalimbali kuanzia katika eneo la utengenezaji fanicha na usimamizi wa miradi.

Katika hatua nyingine CPA Kasole  amesema inajivunia mageuzi makubwa iliyoyafanya katika sekta ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini ambayo yamewezesha Watanzania wengi kujiajiri na  kuajiriwa.

“Kwa sasa VETA  tunatoa ujuzi katika maeneo mbalimbali ikiwemo kwa wale watu wanaohudumia wazee .majumbani , takribani watu 700 wameweza kuhitimu mafunzo  na kupata ajira”amesema CPA Kasole

Aidha amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa kuweza kuweka msisitizo katika elimu ya mafunzo na Ufundi stadi .

Amesema kupitia msisitizo huo VETA wameweza kuona manufaa makubwa sana  na kuweza kufaidika na kutekeleza mambo mengi .

“Kwa sasa VETA ina vyuo  80 nchini na 65  vinakwenda kumaliziwa na Serikali…Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi vyuo hivyo ambao  upo katika hatua nzuri ya ukamilishaji wa awamu ya kwanza”amesema 

Mkurungezi Mkuu huyo amesema kukamilika kwa vyuo hivyo VETA itakuwa na jumla 145 hapa nchini katika kila wilaya ambayo vinakwenda kuwasaidia wananchi kupata elimu na ujuzi wanaotaka Kwa urahisi.