TRA KUTOA HUDUMA YA TIN VIWANJA VYA SABASABA

Na Aziza Masoud,Dar es Salaam

MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewataka wananchi wanaohitaji  kuhudumiwa masuala mbalimbali yakikodi  ikiwemo namba ya utambulisho wa biashara (TIN) kufika katika viwanja vya Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Sabasaba kuweza kupata huduma hiyo

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 30, 2025 Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa TRA,Richard  Kayombo  alisema wameshiriki  katika Maonesho hayo  ya 49 kwa ajili yakuendeleza kutoa elimu ya kodi kwa wadau  wanaofika katika viwanja hivyo.

“Tumeona tuje ili kuwaelimisha wadau mambo.mapya na ya zamani kama kuhusu Chuo chetu cha kodi,vivutio vya kodi,sekta za kilimo  pia ukija bandana kwetu utapata huduma ya kupata  TIN namba hapa hapa bandani,I”alisema Kayombo.

Alisema  katika maonesho hayo mamlaka ina mambo mengi ikiwemo kuwaelekeza watu kuagiza bidhaa,kuwaelekeza bidhaa zenye misamaha ya kodi.

Alisema watembeleaji pia wataelekezwa jinsi ya kutoa taarifa kwa wafanyakazi wasio na maadili ili waweze kuchukuliwa hatua.

“Wateja pia tutawaelewesha jinsi ya kuwaripoi  wafanyakazi ambao hawana maadili na tunawaelimisha tunachukua hatua gani kwa watu hao ili waweze  kufanya kazi kwa  maadili,”alisema Kayombo.

Alisema katika banda hilo  kuna huduma za stampu za kodi  kwa wateja na elimu ya a kupata elimu bidhaa zipi zinatakiwa kuwekwa stempu.

Alisema katika banda hilo pia kuna watalaam wakuelewesha kuhusu  bidhaa bandia  ambapo wateja watapata elimu hiyo kwa upana.