Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam
SHULE za Green Acres imefanya ziara na kutoa msaada wa vitu mbalimbali kwa ajili yakuwasaidia wagonjwa waliojifungua,wenye watoto njiti na waliolazwa kwa sababu mbalimbali katika wodi ya watoto hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala.
Msaada huo ni sehemu ya sherehe za maadhimisho ya miaka 25 tangu kaunzishwa kwa shule hizo mwaka 2000.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Mkurugenzi wa Shule za Green Acres,Jacklyne Rushaigo alisema shule hizo kama wametembelea na kutoa msaada kwa hospitali hiyo kama sehemu ya kurudisha kwa jamii kutokana kutoa huduma ya elimu kwa jamii ya Watanzania kwa muda mrefu.
“Kama taasisi ya elimu inayojali maadili, utu na huduma kwa jamii, tumetembelea wodi ya watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwananyamala ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 25 tangu kuanzishwa kwa shule hizo,”amesema Rushaigo.

Amesema ziara hiyo imelenga kuwafariji watoto waliolazwa kwa kuwapatia sadaka pamoja na ujumbe wa matumaini na upendo kutoka kwa wanafunzi wetu.
Katika ziara hiyo waliambatana na mdhamini mkuu wa sherehe za Maadhimisho ya shule benkiya CRDB ambayo imekuwa kinara katika kutambua na kujali vijana katika sekta ya elimu,ambapo Meneja wa benki hiyo Kanda ya Pwani Badru Idd alisema ushiriki wao katika maadhimisho ya Green Acres ni muhimu kwakuwa benki hiyo pia inafikisha miaka 30 mwaka huu.

“CRDB tumeungana na Green Acres kuja hapa Mwananyama kutoa mkono wa asante kwa wateja na jamii ambayo tunaifanyoa kazi,”amesema Idd.
