KAPINGA:MITAA 58 HALMASHAURI YA MJI WA TARIME IMEFIKIWA NA UMEME

Na Mwandishi Wetu,Dodoma

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali imefikisha  umeme kwenye mitaa 58 ya Mji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kati ya mitaa 81 ya Halmashauri hiyo.

Kapinga ameyasema hayo leo Mei 26, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Tarime Mjini, Mhe. Michael Kembaki aliyeuliza Serikali itapeleka lini umeme katika mitaa 18 ya Halmashauri ya Mji wa Tarime. 

“Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime ina mitaa 81, kati ya hiyo mitaa 58 tayari  imefikiwa na umeme, na mitaa 23 bado haijafikiwa na umeme.”  Amesema  Kapinga

Ameongeza kuwa, mitaa 13 inapelekewa umeme kupitia mradi wa Hamlets Electrification Project – IIA (HEP IIA) unaotekelezwa na Mkandarasi Dyname Construction Engineering,  na mitaa 10 iliyobaki itafikishiwa umeme katika miradi inayofuata.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Wanawake (UWT), Zaytuni Swai aliyeuliza kuhusu jinsi  Serikali ilivyojipanga  kupeleka umeme maeneo ya pembezoni mwa mji wa Arusha hususan kwenye Kata ya Telat, Kapinga ameeleza kuwa, Serikali inatekeleza miradi mbalimbali katika maeneo ya pembezoni  (Peri Urban)  kupitia Wakala wa Nishati Vijijini  (REA) ambayo lengo lake ni kusambaza  umeme maeneo ya pembezoni mwa mji.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum,Cecilia Pareso alyeuliza kuhusu Vitongoji vya Wilaya ya Karatu kutokuwa na umeme na vichache vilivyo kwenye mradi kupelekewa nguzo 40 ambazo hazitoshelezi mahutaji na kuiomba Serikali  kuongeza idadi hiyo, Kapinga amesema kuwa kwa kawaida miradi ya Vitongoji inawigo kulingana na kazi aliyopewa  Mkandarasi.

Hata hivyo amesema  kuwa Wilaya ya Karatu ipo katika mradi wa Vitongoji 9,000 ambao utaanza kutekelezwa hivi karibuni na kusisitiza kuwa, miradi ya kupeleka umeme kwenye Vitongoji ni endelevu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *