KAILIMA AWATAKA WANANCHI WAJITOKEZE KUHAKIKI, KUBORESHA TAARIFA ZAO TABORA

Na Mwandishi Wetu, Tabora.

MKURUGENZI wa Tume Huru ya Uchaguzi, Ramadhani Kailima amewataka wananchi wa Mkoa wa Tabora kujitokeza kuhakiki na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kwenye vituo walivyojiandikishia na kutazama daftari la awali lilolowekwa wazi na kutoa taarifa za wale waliokosa sifa kuwepo kwenye daftari hilo

Kailima amezungumza hayo Mei 4, 2025 wakati alipokuwa anatembelea na kukagua vituo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ambapo amesema wananchi wameonesha mwitikio mkubwa kwa kujitokeza kuhakiki taarifa zao.

Alisema Tume imeweka wazi daftari la awali la wapiga kura katika vituo vyote vilivyotumika kuandikisha na kuboresha taarifa za wapiga kura katika awamu ya pili hivyo wananchi wajitokeze kuhakiki taarifa zao na kutoa taarifa za wale ambao hawastahili kuwepo katika Daftari hilo.

“Wananchi endapo wataona katika Daftari ambalo tumeliweka katika kila kituo kuna mwananchi ambaye amekosa sifa kama vile kufariki basi wawe huru kwa kutumia fomu namba 5B kumuondoa huyo ambaye amekosa sifa za kuwepo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,” alisema Kailima.

Aliongeza kuwa, Mkoa wa Tabora unavituo vya kujiandikishia daftari la mpiga kura vipo 376 mkoa mzima. Hata hivyo, alisisitiza wananchi waendelee kujitokeza katika kuboresha taarifa zao wale ambao hawakuboresha taarifa zao katika awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura basi ndio kipindi cha kafanya hivyo.

Aidha, tume inatoa nafasi kwa watu wote wenye changamoto ya kutoa kuona kusikia na kutoajua kusoma wanatakiwa kuja na watu wao wenye uwezo wa kuwasaidia ili waeze kujiandikasha kwenye Daftari la mpiga kura .

Kwa upande wake, Mratibu wa Uandikishaji Mkoa wa Tabora, Elihuruma Nyella alisema hali ya uandishikishaji katika Mkoa wa Tabora unaendelea vizuri na watu wanajitokea.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili unafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura kuanzia Mei 01, 2025 na kukamilika tarehe 07, 2025 katika mikoa 15 ya mzunguko wa kwanza katika awamu ya pili ya uboreshaji.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *